Wednesday 26 March 2014

WATUMISHI WA MUNGU WATUMIE PIA ELIMU YAO KUIKOMBOA JAMII.

Leo ndugu wadau nimeona niwape kisa ambacho natumai kwa watakao nielewa kitawasaidia.

Mahali flani kulikuwa na wanakijiji ambao maji yao yote ya kijiji hicho walikuwa wanayapata kwenye msitu mmoja ambao ulikuwa unapatikana kwenye kijiji hicho.

Ndani ya msitu huo inasemekana kuna nyoka mkubwa sana ambaye ndiye aliyesadikika kuwa ndiye chanzo chote cha maji ya kijiji hicho,kwahiyo wazee wa kijiji hicho walikataza kabisa mtu yeyote asije akakata mti ndani ya msitu ule maana watu wakiwa wanakata miti basi nyoka huyo atakasirika na kutotoa maji tena na huenda akahama kijiji hicho.
Miaka nenda rudi msitu huo haukukatwa mti kamwe na kuacha uoto wa asali wa msitu huo kuendelea kukua vizuri siku hadi siku.

Baada ya miaka kadhaa,mtumishi wa MUNGU aliweza kuhamia na kuanza kuishi ndani ya kijiji hicho.Kutokana na hali ya maji ya kijiji kile ilivyo na chanzo chake kama inavyosemekana kuwa ni yanaletwa na nyoka huyo mkubwa,mtumishi huyo hakupendezwa na hiyo hali kutokana na imani aliyonayo.Mtumishi huyo aliona haimpendezi kabisa kutumia maji hayo kwa vile inasemekana yanatolewa na nyoka wa msitu huo.

Mtumishi huyo aliona imefika wakati wa kutomtukuza nyoka huyo bali ni MUNGU pekee,kwahiyo aliwapa somo wanakijiji na wakapanga kwenda kukata miti yote iliyokuwa inapatikana ndani ya msitu huo ili kama sio kumuua huyo nyoka basi wamfukuze kabisa kwasababu ni roho chafu kulingana na imani yao na hapaswi kutukuzwa.

Wanakijiji wakishirikiana na mtumishi wa MUNGU waliweza kukata miti yoote ya msitu ule na kuona kuwa wameishinda nguvu hiyo ya giza.

Baada ya miaka kadhaa,kijiji hicho kikaanza kukosa maji kabisa,baada ya wazee na baadhi ya watu kukaa na kuwaza kwanini,jibu walilolipata ni kwamba mtumishi yule na watu alioshirikiana nao kukata miti ya msitu ndio chanzo cha ukosefu wa maji katika kijiji hicho.

Miaka ilizidi kwenda bila kijiji kupata maji na matokeo yake wanakijiji wakaamini kuwa ni kweli kwamba kufukuzwa kwa yule nyoka ndani ya msitu kulikosababishwa kukatwa kwa miti yoote ndio kumemfanya akasirike na kuwakosesha maji.

Mtumishi wa MUNGU hakujua lengo la wazee walioweka sheria hiyo walikuwa na maana kubwa sana.
Walijua miti ikikatwa itasababisha ukame na walifanya hivyo ili kuwatisha watu wakijua watatii na kutokata kabisa miti iliyopo ndani ya msitu huo.



Kama mtumishi wa MUNGU, unatumiaje elimu yako ya kiroho na kidunia katika kuwaelimisha na kuwakomboa wananchi kulingana na eneo ulilopo????


No comments:

Post a Comment