Tuesday 4 March 2014

KADINALI PENGO ATOA MSIMAMO WAKE BINAFSI KUHUSU MFUMO WA KUPIGA KURA KWENYE BUNGE LA KATIBA

Akiongea leo na waandishi wa habari,tarehe 4~3~2014,Askofu Mkuu wa kanisa katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo amesema kama kanisa halijasema chochote kuhusu mfumo wa serikali kama linavyozushiwa kuwa,kanisa la katoliki linataka serikali mbili ndio ziwepo.
Amesema huo sio msimamo wa kanisa na wala kanisa halijasema chochote kuhusu hilo swala.

Kwa upande mwingine,Kadinali Pengo amegusia kuhusu swala la upigaji kura unaotakiwa kutumika katika bunge la katiba linaloendelea hapa nchini Tanzania,mkoani Dodoma.Ili kueleweka zaidi aliamua kutoa mfano huu,

"Mimi nikiwa na bosi wangu na likaulizwa swali,lazima nimwache bosi wangu anyooshe kidole kwanza na kujibu ili mimi nifuate,maana kama nitakuwa tofauti nae,nitahofia kupoteza kazi yangu ofisini.Kwahiyo mimi binafsi na siyo kama kanisa,napendekeza mfumo wa kura ya siri utumike."

Alisema Kadinali Pengo akiongea na waandishi wa habari.





SOURCE: ITV

No comments:

Post a Comment