Friday 7 March 2014

MAPAMBANO DHIDI YA MOJA WA ADUI WA TANZANIA BADO HAYARIDHISHI.

Ndugu wadau wa blog hii,nilishawahi kupost habari hii,kupitia PAGE yangu iitwayo "Save Societies" iliyopo facebook mda mrefu lakini nimeamua kuileta tena ili watu ambao hawakupata fursa kuipitia waweze kuisoma.

Tanzania ina maadui wakubwa 3,ambao ni UJINGA,UMASIKINI na MARADHI.

Hapa nimeamua kumuonesha adui mmojawapo anaesumbua sana nchi yetu ya Tanzania.

Hebu karibu usome ili unielewe zaidi.



Katika hali isiyo ya kawaida,shule moja wilayani Bagamoyo imekutwa ikiwa na mwalimu mmoja tu
anayefundisha wanafunzi kuanzia chekechea hadi darasa la saba,wote wakifundishwa katika chumba
kimoja kwa kutumia ubao mmoja.

Hata hivyo,katika matokeo ya darasa la saba mwaka jana,wanafunzi wote 12 walifaulu kuingia kidato cha kwanza.
Shule hiyo ya msingi Machala, iliyokuwa na idadi ya wanafunzi 198 imejengwa kwa majani kuanzia
chini hadi kwenye paa.

Mwandishi wa habari hizi aliyetembelea shule hiyo, alimkuta mwalimu huyo akiwafundisha wanafunzi hao wa madarasa tofauti wakiwa kwenye chumba kimoja,huku ubaowakufundishia ukiwa umechorwa
mistari mitatu kutenganisha masomo ya chekechea hadi darasa la pili,mstari mwingine darasa la tatu hadi la tano na mwingine darasa la sita hadi la saba.

Mwalimu huyo,Christopher Rukutu,aliliambia NIPASHE kuwa shule hiyo hutumia kivuli cha mti kama ofisi.

Shule hiyo iliyopo katika kijiji cha Mihunga Kata ya Miono,Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani,ilianzishwa na serikali tangu mwaka 2007 ikiwa na wanafunzi 12 ambao wamemaliza darasa la saba,mwaka jana na kubahatika kufaulu wote.

Kwa mujibu wa mwalimu Rukutu,wanafunzi wote waliofaulu walipata alama za A na B isipokuwa mmoja aliyepata alama C.

Pamoja na kuwa katika mazingira magumu,shule hiyo kiwilaya ilishika nafasi ya sita na kimkoa nafasi ya 20.

Alisema shule hiyo haina vitabu vya kiada wala vya kufundishia na amekuwa akiazima kutoka shule za jirani.

SOURCE: NIPASHE

NINI MAONI YAKO???








No comments:

Post a Comment