Kama wazazi tena wanao wajali watoto wao,lazima wahakikishe watoto wao wanapata mahitaji muhimu ya kijamii kama chakula,malazi na makazi mazuri.
Lakini katika maswala yoote ya malezi kwa watoto,usafi pia ni swala muhimu sana.Kama mzazi/mlezi inakupasa uhakikishe mtoto au watoto unaowalea mda wote wanakuwa kwenye mazingira ya usafi.
Kuwaacha watoto kuwa wachafu kutasababisha magonjwa mengi sana kwenye miili yao na hatimae kuumwa na kuidhoofisha miili hiyo.
Vilevile,kutaweza kukusababishia gharama kubwa za matibabu pindi pale watakapoanza kuumwa.
Kumbuka kinga ni bora kuliko tiba.
Licha ya hivyo uchafu huleta aibu kwenye jamii inayokuzunguka.Unapo waacha watoto wako wawe wachafu,usifikiri lawama zote zitakuwa kwao tu bali hata kwako mzazi/mlezi, maana utaonekana huwajali watoto wako na kuonekana hovyo mtaani.
Ifike mahali usafi wa miili na mazingira usiwe tu kwa wazazi/walezi pekee,bali hata kwa watoto wao wanao walea.
No comments:
Post a Comment