Wednesday 12 March 2014

MATOKEO YA MWENYEKITI WA KUDUMU WA BUNGE LA KATIBA YATANGAZWA.

Msimamizi wa uchaguzi wa mwenyekiti wa bunge maalumu la katiba,ameweza kutangaza matokeo ya mwenyekiti wa kudumu wa bunge hilo.

Katika mchuano huo walikuwa wagombea wawili ambaye wa kwanza ni Mh. Samweli John Sitta pamoja na Mh. Hashim Rungwe.

Katika uchaguzi huo,

Kura zilizopigwa ni 629

Wapiga kura wote walikuwa 563

Zilizoharibika ni 7

Katika kura hizo Mh. Hashim Rugwe alipata kura 69 na Samwel Sitta alipata kura 487.

Kwa matokeo hayo Mh. Samweli Sitaa kaibuka na ushindi wa kuwa mwenyekiti wa kudumu wa bunge maalumu la katiba.

Mh. Samweli Sitta atapokea kiti hicho kutoka kwa mwenyekiti wa muda wa bunge maalumu la katiba, mh. Pandu Amir Kificho.

Katika pongezi zake mh. Sitta ameahidi utendaji kazi kwa uadilifu na kasi.


UCHAGUZI WA MAKAMO MWENYEKITI WA BUNGE MAALUMU LA KATIBA.

Katika upande mwingine,mwenyekiti wa muda wa bunge maalumu la katiba,mh. Pandu Amir Kificho,ameweza kutoa ratiba ya uchaguzi wa makamo mwenyekiti wa bunge maalumu la katiba utakaofanyika kesho tarehe 13/4/2014, saa 10 jioni.

Katika sheria iliyopo sasa inasema mwenyekiti akitokea Bara basi makamo wake anatakiwa atokee Zanzibar.Pia kama mwenyekiti atakuwa mwanaume basi makamo wake anatakiwa awe mwanamke.

Na uchaguzi uliomalizika leo na kumfanya Mh. Samweli Sitta kuwa mshindi,utafanya kwa sasa makamo wake awe mwanamke na atokee Zanzibar.

Fomu za kugombea zitatolewa leo mara baada ya kikao cha bunge kuisha kwenye ofisi ya baraza la wawakilishi.

Mgombea yeyote anatakiwa awe na wadhamini wasiopungua 20 yaani 10 kutoka bara na 10 wengine kutoka Zanzibar. 

Fomu zote zitatakiwa kurudishwa kesho sa 4 asubuhi kwenye ofisi hizohizo.



sitta

No comments:

Post a Comment