Friday 28 February 2014

TANZANIA KAMA NCHI,IMEJIPANGAJE KUKATAA MISAADA INAYOTOLEWA NA MATAIFA TAJIRI AMBAYO INAKUJA NA MASHARTI YENYE SERA ZA USHOGA??

Rais wa Uganda Yoweri Museveni ametia saini mswada wenye utata unaotoa adhabu kali kwa watakaopatikana wakishiriki mapenzi ya jinsia moja.


Rais Museveni alitia saini mswada huo nyumbani kwake katika hafla iliyoshuhudiwa na maafisa wakuu wa serikali pamoja na wandishi wa habari.
Mswada huo ambao sasa utakuwa sheria, unatoa adhabu ya kifungo cha maisha jela kwa wale watakaopatikana na hatia ya kuhusika na mapenzi ya jinsia moja.


Mswada huo pia umeharamisha wanaharakati kutangaza misimamo yao hadharani kuhusu au kuwasaidia wanapenzi wengine wa jinsia moja kujitangaza hadharani.

Adhabu hiyo pia itatolewa kwa wale wanaopatikana na hatia ya kuwahusisha watoto katika vitendo hivyo, walemavu au kumuambikiza mtu virusi vya Ukimwi katika mapenzi ya jinsia moja.

Mswada huo umepigiwa debe sana nchini Uganda, lakini mashirika ya kimataifa ya kutetea haki za binadamu yameulaani.
Uganda imepuuzilia mbali shinikio za Marekani na nchi zengine za Magharibi kutopitisha sheria kali dhidi ya vitendo vya mapenzi ya jinsia moja.

Mswada huo umeweka sheria kali zaidi dhidi ya uhusiano wa mapenzi ya jinsia moja kwa yeyote atakayepatikana akishiriki.

Usagaji pia umeharamishwa kwa mara ya kwanza na pia ni hatia kumsaidia mtu kushiriki mapenzi ya jinsia moja. Wanaharakati wa kutetea haki za wapenzi wa jinsia moja wanasema wanajiandaa kwenda mahakamani kupinga sheria hiyo mpya.

Uganda ni miongoni mwa mataifa 30 Afrika ambayo yameharamisha mapenzi ya jinsia moja. Ni wiki jana tu ambapo Rais wa Gambia Yahyah Jammeh aliyesema mapenzi ya jinsia moja ni sumu kali mno.





Benki ya dunia imebana msaada wa dola milioni 90 kwa Uganda , siku chache tu baada ya Rais Yoweri Museveni kuishinisha sheriua mpya dhidi ya mapenzi ya jinsia moja.

Benki hiyo imesema kuwa inataka kufanya tathmini yake kuhakikisha kuwa malengo yake ya maendeleo nchini Uganda katika sekta ya afya, ambayo msaada huo ulikuwa unanuiwa, hayataathirika .

Sheria iliyoidhinishwa na Rais Yoweri Museveni, ilitiwa saini Jumatatu na inatoa adhabu kali kwa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja.

Wafadhili wengine tayari wameanza kusitisha misaada Uganda. Wahisani kama Denmark na Norway wamesema kuwa wataanza kufadhili mashirika moja kwa moja badala ya serikali.
Aslimia 20% ya bajeti ya Uganda inategemea michango ya wafadhili.


Mpaka sasa nchi tatu za Ulaya zimeamua kukata misaada yao kwa mamilioni ya dola.
Wizara ya fedha ya Uganda imesema inasubiri mawasiliano rasmi ya nchi husika, na iko tayari kukabiliana na athari za hatua hiyo.

Hadi kufikia sasa Waziri wa Fedha Wa Sweden, akiwa mjini Kampala, alisema wawekezaji kutoka nchi yake watakuwa na wakati mgumu kuweka pesa zao nchini Uganda kwa sababu watakuwa na hofu kuwa sheria yo yote inaweza kupitishwa kuwadhulumu watu.

Jana serikali ya Uholanzi ilisema itazuia kwa muda misaada kwa Serikali ya Uganda. Norway na Denmark pia zimetangaza kupunguza au kusimamisha kwa muda misaada yake kwa Uganda.





Marekani haikufurahishwa na hatua ya Uganda kuidhinisha sheria dhidi ya wapenzi wa jinsia moja.


Waziri wa mashauri ya Kigeni wa Marekani, John Kerry amesema tangu Uganda iidhinishe mswada huo miaka minne iliyopita, Marekani ilieleza wazi kwamba sheria hiyo inakiuka jukumu la kuhakikisha kuwepo haki za binaadamu ambalo tume ya haki za binaadamu Uganda inatambua linaambatana na sheria ya Uganda.

Kerry amesema,' Baada ya kuidhinishwa sheria hii, tunaanza ukaguzi wa ndani wa uhusiano wetu na serikali ya Uganda, kuhakikisha kwamba pande zote za uhusiano wetu, ukiwemo miradi ya msaada, zinapinga sera na sheria zinazowaonea watu na tuwe na uhusiano unaodhihirisha maadili yetu'

Tamko hilo limetolewa siku moja baada ya rais Yoweri Museveni kukaidi shinikizo la kimataifa na kutia saini sheria hiyo iliyo zusha mzozo, inayoharamisha mapenzi ya jinsia moja Uganda, hatua iliyozusha hisia kali.

Baadhi ya mataifa ya magharibi tayari yanatishia kukatiza msaada wa moja kwa moja kwa serikali ya Uganda.



John Kerry
Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Amerika John Kerry.




Marekani inasema kuidhinishwa kwa sheria hiyo kunatishia hatari ya kurudi nyuma katika uwajibikaji wa Uganda kulinda haki za raia wake na kutishia jamii ya wapenzi wa jinsia moja Uganda.


Waziri wa mambo ya nje nchini Uganda, Sam Kutesa amesema ana wasiwasi kuwa Marekani huenda ikasitisha msaada wake kwa taifa hilo baada ya Rais Yoweri Museveni kuidhinisha sheria dhidi ya ushoga nchini humo.
Bwana Kutesa amesema kuwa watu sharti wawe na maadili na kukubali msaada.
Balozi wa Marekani nchini Uganda Scott DeLisi, awali aliitaka serikali ya Uganda, kubatilisha sheria hiyo.
Alisema alihitaji kufafanuliwa zaidi sheria hiyo, kabla ya Marekani kujua ikiwa itaendelea na mipango yake ya misaada kwa nchi hiyo hasa miradi ya kupambana dhidi ya HIV na Ukimwi..

Sheria hiyo mpya, inatoa adhabu kali kwa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja na kupiga marufuku kile inachosema kusambaza vitendo vya ushoga.






SOURCE: BBC SWAHILI



Hivyo ndivyo vikwazo walivyoanza kuvipata jirani zetu wa Uganda.

Tanzania kama nchi ambayo bajeti yake kubwa inategemea fedha za hao hao wafadhili kutoka nchi za magharibi amabazo ndio sera zao kubwa ni kuunga mkono ndoa za jinsia moja, imejipanga vipi kukabiliana na hilo????


Leo hii,viongozi wana mikakati gani kuimarisha uchumi ili swala la ushoga lisije likaharibu maadili ya nchi yetu???


Ni vyema kama taifa likaanza sasa maana wahenga wanasema,Ukiona Mwenzio Ananyolewa,Wewe Tia Maji.

Wednesday 26 February 2014

UZINDUZI WA KAMPENI YA UELEWA WA RASIMU YA KATIBA WAKAMILIKA

Leo tarehe 26/2/2014,ndani ya ukumbi wa Mlimani City,uliopo jijini Dar Es Salaam,kumeweza kufanyika rasmi Uzinduzi Wa Kampeni ya Uelewa wa Rasimu ya Katiba.

Uzinduzi huo umeweza kuwashirikisha wadau mbalimbali kama LHRC,wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa kituo hicho cha sheria na Haki za Binadamu, Dr Helen Kijo-Bisimba, Policy Forum,SHIVYAWATA,TYC na National Council Of NGOs (NaCoNGO), TUCTA,Jukwaa La Katiba,TAWLA,TAMWA n.k.

Uzinduzi huo uliweza kuzindua mambo yafuatayo:

  • Kipeperushi cha mambo 7 makubwa mapya ya kuungwa mkono na wananchi katika rasimu ya katiba na mambo makubwa 5 yanayokosekana katika rasimu ya katiba.
  • Chapisho la lugha nyepesi
  • Tovuti tofauti tofauti
  • CDs na flash kwaajili ya kusikiliza rasimu ya katiba
  • Chapisho la nukta nundu kwa walemavu (Maandishi yanayosomwa na watu wasioona),na mambo mengine mengi
Katika swala la tovuti,wameweza kuzindua tovuti ifuatayo ambayo kwa sasa kila mtu popote alipo duniani ataweza kusoma vizuri mambo yanayoendelea kwenye mchakato wa kuipata katiba mpya.

Tovuti hiyo ni, http://www.taifaniletu.blogspot.com/

Pia wameeleza kwa baadae kidogo watakuwa na tovuti iitwayo www.sikilizarasimu.com ambayo nayo itasaidie kuelewa mabo yote ya rasimu ya katiba mya.


Wameeleza pia wataweza kuzunguka nchi nzima katika kutoa elimu ya maswala ya katiba kila mkoa ndani ya kata 3 za kila wilaya zenye watu wengi na kisha kuwasambazia watu wengine.



Monday 24 February 2014

HUYU SIYO YESU KRISTO WA NAZARETH KAMA WAKRISTO WENGI WANAVYOAMINI.

Leo nimeona niwaletee makala hii inayohusu imani za wakristo wengi na wale woote wanaoamini kuwa mwigizaji Brian Deacon,ndiye YESU KRISTO.Lengo ni kuwasaidia wale wanaoamini hivyo kuacha kuamini huko kwasababu YESU mwenyewe siyo huyu anayejulikana kwa watu wengi hapa duniani.
Ifuatayo ni historia ya maisha yake;




Brian Deacon ndio jina lake mwigizaji huyo ambaye ni mwingereza aliyezaliwa mnamo tarehe 13/02/1949 huko Oxford nchini Uingereza akiwa ni mtoto wa pili katika familia yao baba yake akiwa fundi makenika na mama yake akiwa ni nesi.

Ndoa yake ya kwanza na Rula Lenska ilivunjika ambapo alizaa na mkewe huyo binti yao aitwaye Lara Deacon,ndoa yake ya pili alioana na mwanamama Natalie Bloch mnamo mwaka 1998 mpaka sasa wapo kwenye ndoa hiyo.

Brian Deacon ndani ya filamu ya ''JESUS''
Aliigiza filamu ya Yesu ambayo pia ilimfanya aokoke mara baada ya kuitazama akiwa na miaka 30,baada ya kupita kwenye mchujo mkali wa waigizaji zaidi ya elfu moja ambao walifanyiwa mahojiano huku 260 wakijaribishwa kuigiza(screen test)kuona kwamba wanafaa akiwa ni mwingereza pekee kati ya waigizaji Waisrael walioingia kwenye usaili huo akiwa chini ya kampuni iitwayo New shakespears ambako alikuwa akifanya sanaa za majukwaani na uigizaji.


Brian Deacon miaka iliyofuatia baada ya kuigiza kama Yesu.

Amesema kabla ya kuchaguliwa mtihani wake wa kwanza ulikuwa kutoka kwa wakala wake aliyemvunja moyo kwakumweleza hadhani kama yeye(Brian)atafaa kwenye kumwigiza Yesu,lakini anasema alifanikiwa,baada ya hapo akawa na wakati mgumu kutoka kwa watu ambao kila mmoja alikuwa anajaribu kumweleza jinsi anavyotakiwa kuigiza,sauti yake na mambo mengine,ingawa yeye alisema nitatumia sauti yangu na maelezo kutoka kwa muongozaji.

Amesema wiki tatu kabla hawajaanza kurekodi filamu hiyo alisoma kitabu cha Luka mtakatifu zaidi ya mara 20 kwakuwa filamu hiyo imenukuliwa kutoka kitabu hicho ambapo Brian amesema kusoma kwake kulimpa nguvu sana na moyo wa kuigiza filamu hiyo na kuweza kumfahamu vyema Yesu kuwa ni mtu wa aina gani.

watu wakiangalia filamu ya Yesu ambayo bwana Brian Deacon ni mwigizaji mkuu.

Katika miezi saba waliyochukua kuigiza filamu hiyo Brian amesema,walikuwa wanaigiza kwa masaa mengi kuanzia saa kumi za alfajiri mpaka mwisho wa siku kiasi kwamba wakati mwingine aliwaambia wenzake kwamba wamsaidie kwani amechoka sana hajui kwamba angeweza kuigiza kwa siku hiyo lakini anasema alikuwa anashangazwa na nguvu za ajabu alizokuwa akizipata na kuendelea kuigiza ingawa wakati huo nasema alikuwa mkristo jina wa kanisa katoliki,alikuwa anauwalakini kuhusu mafundisho na huduma ya Yesu kwa ujumla,siku moja wakati anaigiza alikuwa anawaombea watu mara mwanamke mmoja alishika mkono wake kumbe alikuwa na mapepo alimuombea na mapepo yalimtoka mwanamama huyo.

Siku nyingine waliokuwa wakiigiza kama wanafunzi wa Yesu wapatao 12 wakiwa ndani ya basi walikuwa wamepanga kugoma kutokana na malipo waliyokuwa wakipata cha ajabu Brian anasema director alikuja kumuomba yeye(Brian)azungumze nao warejee kazini akashangaa akamwambia mimi sio Yesu ni Brian Deacon,akaamua kuzungumza nao,baada ya masaa 36 walikubali kurudi kuendelea na kazi

Amesema mtihani mwingine ni siku alipokuwa hotelini Tel Aviv ghorofa ya 18 usiku mara kukawa na moto hotelini hapo baada ya mwingereza mmoja aliyekuwa akivuta sigara kusahau kuizima hivyo kusababisha moto,lakini anasema bahati nzuri hakuna aliyejeruhiwa ila walifanya kazi siku inayofuatia muda mrefu bila muongozaji kujali kwamba hawakulala vyema usiku.






watumishi wa Mungu wakiwa njiani kwenda kuonyesha filamu ya Yesu katika uinjilisti huko Kongo.



Amesema siku hiyo mmoja wa waigizaji anayeitwa Tom Panella alianzisha mada kwa kusema moto uliokuwa umetokea ni hila za shetani,na kusababisha mjadala wa muda mrefu ni vipi shetani anahusishwa kwenye swala hilo lakini jibu likawa,shetani hataki filamu hiyo irekodiwe ndio maana analeta hila zake.haikuwa kazi rahisi kurekodi filamu hiyo na pia si ujuzi wa kufurahia,baada ya kumaliza kurekodi kwa takribani miezi 18 ilianza kuonyeshwa kwa baadhi ya watu na ndipo hata yeye kwa mara ya kwanza akaona ni kwa jinsi filamu hiyo ilivyonanguvu,ukweli na kugusa mioyo ya watu.

Baada ya filamu hiyo Briana anasema alirudi kuigiza majukwaani na kwenye runinga, ambapo kwa miaka zaidi ya 30 sasa tangu kutoka filamu ya Yesu tayari imetazamwa na watu zaidi ya bilioni tatu katika nchi 233(kwa takwimu za mwaka 2001),zaidi ya watu milioni 117 waliamua kubadilisha maisha yao na kumpokea Yesu,filamu hiyo ambayo ilitengenezwa chini ya Campus Crusade for crusade ambao kwasasa wanaitwa Life Ministry pia nchini Tanzania wapo chini ya mkurugenzi Dismas Shekhalage.ambapo tayari imetafsiriwa katika lugha zaidi 500 huku nyingine zaidi ya 200 zikiwa njiani kutafsiriwa.

Brian anawaambia watu kwamba yeye ni mwigizaji tu na sio Yesu kama watu wengine na kuwataka watu hao kujua hivyo ambapo anasema ameendelea kupata barua mbalimbali za kumpongeza na kumshukuru kwa kazi nzuri aliyofanya kwenye filamu hiyo,ambapo kwa upande wake anasema anayo nakala ya filamu hiyo kwenye maktaba yake nyumbani kwao Uingereza,ambapo kwa takribani miaka 20 filamu hiyo imekuwa ikitazamwa duniani kote na kubadilisha maisha ya watu.

kati ya filamu alizowahi kushiriki ni pamoja na A zed & Two Noughts ya mwaka 1985,The Feathered Serpent ya mwaka 1976-1978 na Tamthilia ya iitwayo Lillie iliyoigizwa mwaka 1978 akitumia jina la Frank Miles.

Sunday 23 February 2014

DR. SLAA ATOA TAMKO KUHUSU POSHO ZA WAJUMBE WA BUNGE MAALUMU LA KATIBA MPYA.

Katibu mkuu wa CHADEMA,Dr Slaa,akiwa kwenye mkutano wa kumnadi mgombea ubunge wa chama hicho,jimbo la Kalenga,Grace Tendega,aamua kutoa msimamo wa chama kuhusu posho za wajumbe wa bunge maalum la katiba mpya,

Ananukuliwa akisema,
"CHADEMA hatutakuwa tayari kwa wajumbe wa bunge maalum la katiba mpya kuongezewa posho zaidi ya shilingi 300,000/= (laki tatu),kwakuwa hela hiyo inawatosha kula,kulala na kufanya kazi zao vizuri wakiwa Dodoma.Na endapo watazidishiwa,kama chama,watazunguka kwa maandamano nchi nzima kwaajili ya kupinga upandishwaji wa posho hizo.Kupandishwa kwa posho hizo itakuwa maajabu kwa taifa hili."

Dr Slaa ametoa kauli hiyo jana tarehe 23-04-2014,akiwa jimbo la Kalenga.




460>_3559850




SOURCE: ITV

Friday 21 February 2014

Thursday 20 February 2014

Wakati wabunge wanazidi kupeta,wanataaluma wanazidi kudhalilika kimaslahi

Wakati wabunge wakiendelea kuongezewa posho za vikao, imebainika kuwa fedha anazolipwa mbunge mmoja kwa mwezi ni sawa na mishahara ya mwalimu wa shule ya msingi ya miaka mitatu. Malipo hayo pia yanaonekana kuwa sawa na mshahara wa mwaka mmoja wa daktari msaidizi mwenye shahada moja, anayeanza kazi.
 

Uchunguzi uliofanywa na gazeti la Mwananchi umebaini kuwa mbunge mmoja hulipwa Sh 7.3 milioni kwa mwezi, ikiwa ni jumuisho la mshahara na malipo mengine ikiwamo posho za vikao. Jumuisho hilo ni pamoja na posho mbalimbali kila mwezi kama vile za mafuta ya magari, ubunge, kukaa jimboni, kuendesha ofisi na simu. Posho ya mafuta ni Sh 2 milioni kwa mwezi ikikadiriwa kuwa atatumia lita 1,000 ambazo makisio ni Sh2,000 kwa lita moja. Nyingine ni posho ya kukaa jimboni Sh 800,000, posho ya ubunge Sh1 milioni, kuendesha ofisi Sh 700,000, simu Sh 500,000 na mshahara ni Sh 2.3 milioni.

Kwa mujibu wa uchunguzi huo, wakati mbunge akiwa hayupo bungeni inaelezwa bado analipwa posho hizo pamoja na mshahara na kumfanya ajikusanyie Sh 7.3 milioni kila mwezi. Wakati wa vikao bungeni, posho zao huongezeka ambazo uchunguzi unaonyesha mbunge hupewa posho nyingine za aina tatu; za kikao, kujikimu na usafiri.


Kwa mujibu wa taarifa hizo, posho hiyo ya usafiri hupewa bila kujali kuwa ana posho ya kila mwezi ya mafuta ya Sh 2 milioni. Viwango vya fedha kwa posho anazopewa mbunge anapokuwa Bungeni kila kikao kwa sasa imeongezeka kutoka Sh 70,000 hadi Sh 200,000 ya posho ya kujikimu Sh 80,000 na usafiri Sh 50,000.


Mwalimu Lakini, wakati wabunge wakifurahia neema hizo, uchunguzi wa gazeti hili umebaini kwamba, mshahara wa mwalimu wa shule ya msingi anayeanza kazi, ambaye yupo kwenye daraja la mshahara la TGTS B ni Sh 200,000 kwa mwezi.


Kwa mwalimu wa sekondari mwenye stashahada ambaye yupo kwenye daraja la TGTS C, mshahara wake ni Sh 300,000 huku yule mwenye shahada wa daraja TGTS D analipwa Sh 400,000, mishahara yote ikiwa ni ya kuanza kazi.


Mchanganuo huo unaonyesha kwamba, pia viwango hivyo vya mshahara vilivyoorodheshwa hapo, ni vile ambavyo havijakatwa kodi zozote zile.Kutokana na hali hiyo, mapato ya Mbunge kwa mwezi mmoja yanaweza kumlipa mwalimu mmoja wa shule ya msingi mishahara ya miezi 36 sawa na miaka mitatu.

Mshahara huo pia utaweza kumlipa mwalimu mmoja wa sekondari mwenye stashahada mshahara wa miezi 24, huku yule mwenye shahada akilipwa kwa muda wa miezi 18 kwa mapato ya mwezi mmoja ya mbunge. Fedha hizo zinaweza kumlipa mfanyakazi wa idara nyingine ya umma, ambaye mshahara wake upo kwenye daraja hilo kwa kipindi kama hicho.



MAONI BINAFSI.


Wabunge wetu hapa nchini mishahara yao na posho havitegemei uzoefu wao wa kukaa bungeni kama watumishi wengine wa serikali,mfano WALIMU.Wabunge wamekuwa wakilipwa mishahara sawa hata kama ndio umeingia leo bungeni basi utapokea milion 7.3 kama wenzako uliowakuta kazini ambao walianza miaka mingi iliyopita.

Yaani kupanda kwa mishahara ya walimu kunategemea pia uzoefu alionao kazini na hata kupanda grade yake.Kadiri anavyopanda grade ndivyo mshahara wake unaongezeka.


SWALI
 

  • Kwanini kama UALIMU wanasema ni wito na UBUNGE usiwe hivyo???
  • Kwanini pia kazi ya UBUNGE mishahara yake isiendane na kupanda grade kama kazi ya ualimu au sekta zingine za serikali???

NB:
 

Kama nchi, ifike mahali tuamue kuwalipa vizuri wana taaluma mfano waalimu,madaktari n.k, kuliko wanasiasa.
 

Haiwezekani mtu mwenye taaluma mfano, ya Ualimu au Udaktari anapokea mshahara mdogo sana kuliko mwanasiasa ambaye unakuta ni "darasa la saba au form four failure".Huku ni kuzalilisha sana wanataaluma na kuudharau mchango wao mkubwa kwa mustakabali wa taifa letu.

Kuwapunguzia mishahara pamoja na posho wabunge na wanasiasa kwa ujumla inaweza ikasaidia kazi hiyo ikawa ya wito kama wanavyoitwa waalimu.Pia itasaidia kupunguza wimbi la watanzania wengi kukimbilia kwenye siasa kwa sasa.







Wednesday 19 February 2014

Tembo Wadogo Nao Hatarini Kutoweka.


Jeshi la polisi mkoani Singida,limefanikiwa kumkamata kijana mwenye umri wa miaka 26 ambaye ni mkazi wa Ukombozi iliyopo Singida,akiwa na vipande16 vya meno ya tembo vyenye thamani ya zaidi ya milioni 17.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake,kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Singida SSP Cordula Lyimo,amesema kijana huyo alikamatwa baada ya jeshi la polisi kufanya msako kwenye kizuizi kilichopo kijiji cha Ukimbu wilaya ya Manyoni mkoani Singida.

Kijana huyo ambaye alikuwa ndani ya bus aina ya scania alikutwa na vipande hivyo ndani ya begi lake la nguo katika harakati za kutaka kuwatoroka askari ambapo juhudi zake zilishindwa kufanikiwa baada ya askari hao kumtilia mashaka na kuwahi kumkamata.

Pia amesema kwa sasa majangili wameamua kutumia mbinu mpya ya kuuwa tembo wadogo baada ya wale wakubwa kupungua kwa kasi kama alivyofanya kijana huyo aliyekamatwa.

Kwa sasa jeshi la polisi linaendelea na msako wa mtandao unaohusika na ujangili huo.






Source: ITV

Thursday 13 February 2014

Hatimae Mh. Jenista Mhagama anena kuhusu ajira za walimu wapya.

Kutokana na mengi kuongelewa kuhusu ajira mpya za walimu,ambapo awali waheshimiwa mbalimbali wa wizara husika walikwisha kutoa matamko tofauti ambayo mpaka sasa hayajatimia,naye naibu waziri wa elimu mafunzo na ufundi mh.Jenista Muhagama aamua kunena.


Awali mwaka jana mwishoni, Naibu waziri anayeshughulikia Elimu (TAMISEMI),Kassim Majaliwa,alinukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari na kusema ajira hizo zinategemewa kutoka mwezi wa kwanza 2014,ambapo kauli hiyo haikutimia mpaka sasa mwezi wa pili na hakutoa tena tamko lolote juu ya hilo.


Mwishoni wa mwezi wa kwanza katibu wa Elimu Mafunzo na Ufundi, Prof. Sifuni Mchome,naye alitoa taarifa kupitia kituo kimoja cha TV,yaani EATV,akisema kila kitu tayari na wanasubiri kutangaza tu hizo ajira mpya za walimu,ambapo mpaka sasa pia kauli hiyo bado haijatimia maana ni kama wiki tatu zimeshapita.


Tarehe 11/02/2014,kulikuwa na kikao ambacho kilihusisha wadau mbalimbali wa elimu yaani walimu na wadau wengine wa sekta hiyo.Kikao hicho kiliendeshwa ndani ya ukumbi wa shule ya sekondari ya Lugalo iliyopo manispaa ya Iringa.


Kikao hicho ambacho mgeni rasmi alikuwa mh. Jenista Mhagama kama naibu waziri Elimu,aliweza kusikiliza mengi yanayoikumba sekta ya elimu.Pamoja na mambo mengi yaliyozungumziwa,wadau walitaka kufahamu ajira mpya za walimu zitatoka lini.


Kwa mujibu wa naibu waziri huyo alisema kuwa wale wote wanaosubiri ajira hizo,majina yatatoka tarehe 1/04/2014 kwasababu kwa sasa serikali haina fedha na nyingi zimetumika kwenye maswala mbalimbali ya kitaifa lakini kubwa ni maswala ya katiba mpya.



Kwa maelezo zaidi unaweza ukawasiliana na mdau yeyote wa elimu aliyehudhuria kikao hicho cha tarehe 11/02/2014,shule ya sekondari Lugalo iliyopo manispaa ya Iringa mjini. 



Naibu waziri anayeshughulikia Elimu (TAMISEMI),Kassim Majaliwa.




Profesa Sifuni Mchome,Katibu Mkuu Wizara ya Elimu





Naibu Waziri wa Elimu Mafunzo na Ufundi,Jenista Mhagama

Tuesday 11 February 2014

Kwanini walemavu hawa wamesahaulika???

Mpaka sasa Mh. Rais,Jakaya Kikwete,ameweza kuteua wajumbe wengine 201 kutoka asasi mbalimbali kama za Wafugaji,Wakulima,Walemavu wa ngozi,Wanasiasa,Taasisi za kidini,Wanaharakati mbalimbali n.k, ambao watajumuika na wabunge wengine katika kujadili juu ya uundwaji wa katiba mpya.

Bunge hili la katiba ambalo linategemewa kuanza tarehe 18-02-2014 bungeni Dodoma,lina lengo la  wajumbe kutoa maoni ambayo yanawakilisha wa Tanzania wengi juu ya muundo wa katiba mpya ambayo inategemewa kuanza kutumika 2015.Na baada ya hapo rasimu hiyo ya pili itarudishwa kwa wananchi ili kupigiwa kura za ndio au hapana,yaani wanaikubali au wanapingana nayo???.
Na kama itakubalika basi ndio itakuwa katiba mpya ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Cha ajabu mpaka mchakato wa kuteua wajumbe wa bunge la katiba kukamilika,kundi la walemavu wa masikio (Viziwi),hawakujumuishwa kwenye bunge hilo la katiba mpaka leo hii,tarehe13-02.

Wakiongea jana na ITV,wadau mbalimbali wamelaani kitendo hicho cha Mh. Rais kuwaacha watu hawa.
Vilevile hawakuishia hapo tu,wameongeza kwa kusema hata kwenye kituo cha kurusha matangazo ya bunge TBC 1, huwa wanakoseshwa haki ya kuelewa nini kinachoendelea maana hawawekewi mkalimani wa kuwatafsiria.
Wadau mbalimbali wamehoji kitendo hicho cha kundi hili kusahaulika ni kuwakosesha haki yao ya msingi kama watanzania.

Pia kwa kituo cha kurushia matangazo cha taifa TBC 1,ambacho kinaendeshwa kwa gharama ya pesa za walipa kodi,wanaona serikali haiwatendei haki kwa autoworker mkalimani, maana hata wao kodi wanalipa sawa na watu wengine wa kawaida kwahiyo wana haki ya kujua nini kinachoendelea ndani ya nchi yetu Tanzania.

Nini maoni yako???

Monday 10 February 2014

Mashoga wanaadhibiwa vipi??

Mahusiano ya jinsia moja kule Nigeria sheria zao zinasema ukikutwa utafungwa miaka 14 au wakitumia sharia yaani zile za kiislam huenda wakapigwa mawe hadi kufa.

Vipi sheria za hapa nchini kwetu Tanzania???

Hudhani kama kuna haja ya kuwekwa hili kwenye katiba mpya ili kupunguza au kuondoa kabisa mahusiano haya ja jinsia moja???