Sunday 23 February 2014

DR. SLAA ATOA TAMKO KUHUSU POSHO ZA WAJUMBE WA BUNGE MAALUMU LA KATIBA MPYA.

Katibu mkuu wa CHADEMA,Dr Slaa,akiwa kwenye mkutano wa kumnadi mgombea ubunge wa chama hicho,jimbo la Kalenga,Grace Tendega,aamua kutoa msimamo wa chama kuhusu posho za wajumbe wa bunge maalum la katiba mpya,

Ananukuliwa akisema,
"CHADEMA hatutakuwa tayari kwa wajumbe wa bunge maalum la katiba mpya kuongezewa posho zaidi ya shilingi 300,000/= (laki tatu),kwakuwa hela hiyo inawatosha kula,kulala na kufanya kazi zao vizuri wakiwa Dodoma.Na endapo watazidishiwa,kama chama,watazunguka kwa maandamano nchi nzima kwaajili ya kupinga upandishwaji wa posho hizo.Kupandishwa kwa posho hizo itakuwa maajabu kwa taifa hili."

Dr Slaa ametoa kauli hiyo jana tarehe 23-04-2014,akiwa jimbo la Kalenga.




460>_3559850




SOURCE: ITV

1 comment:

  1. vizuri na support hili kwani kutaka nyongeza zaidi ya hapo ni rushwa

    ReplyDelete